a Kut 7:19; Kut 4:2; Ay 26:12; Isa 14:27; 23:11; 51:15; Yer 31:35; Mdo 7:36; Mwa 41:6; Kut 15:8; 2Sam 22:16; 1Fal 19:11; Ay 38:1; 40:6; Yer 23:19; Nah 1:3; Mwa 8:1; 2Fal 2:8; Za 74:13; 78:13; 114:5; Za 136:13; Isa 63:12
b Hes 33:8; Yos 24:6; Isa 43:16; 63:11; 1Kor 10:1; Kut 3:12; 15:19; Kum 31:6-8; Yos 3:16; 4:22; Neh 9:11; Za 66:6; 77:19; 106:9; Isa 11:15; 41:10; 43:5; 44:27; Isa 50:2; 51:10; 63:13; Yer 46:28; Nah 1:4; Ebr 11:29; Kut 15:8; Yos 3:13
Exodus 14:21-26
21 aNdipo Musa akanyoosha mkono wake juu ya bahari, naye Bwana akayasukuma maji ya bahari nyuma kwa upepo mkali wa mashariki usiku ule wote na kupafanya nchi kavu. Maji yakagawanyika, 22 bnao Waisraeli wakapita baharini mahali pakavu, maji yakiwa ukuta upande wao wa kuume na upande wao wa kushoto. 23Wamisri wakawafuatia ndani ya bahari, pamoja na farasi wote wa Farao, magari ya vita na wapanda farasi. 24 cKaribia mapambazuko, Bwana akaliangalia jeshi la Wamisri kutoka ile nguzo ya moto na ya wingu, akalifadhaisha. 25 dMungu akayaondoa magurudumu ya magari yao, kwa hivyo wakayaendesha kwa shida. Nao Wamisri wakasema, “Tuachane na Waisraeli! Bwana anawapigania dhidi ya Misri.”Wafuatiaji Wazama
26Ndipo Bwana akamwambia Musa, “Nyoosha mkono wako juu ya bahari ili maji yarudiane yawafunike Wamisri, magari yao ya vita na wapanda farasi wao.”
Copyright information for
SwhKC